TBS yahimiza ubora wa bidhaa

WAWEKEZAJI na wazalishaji nchini wametakiwa kutumia huduma za Shirika la Viwango Tanzania (TBS), hususan katika sekta ya vipimo, ili kuimarisha ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Afisa Mkuu wa Metrolojia wa TBS, Joseph Kadenge amesema metrolojia ni msingi muhimu wa ubora, unaohakikisha usahihi wa vipimo katika mashine za uzalishaji.

Ameeleza kuwa ubora wa bidhaa hutegemea usahihi wa mashine, hivyo vipimo visipokuwa sahihi huathiri ubora wa bidhaa. Kadenge ameongeza kuwa TBS ina Maabara ya Taifa ya Vipimo (National Metrology Laboratory) iliyotambuliwa kimataifa kupitia BIPM, pamoja na kupata ithibati ya umahiri kutoka SADCAS.

Amesema huduma za ugezi zinapatikana kwa viwango vya kimataifa, na kuwahimiza wawekezaji kuendelea kuwekeza nchini bila hofu. SOMA: TBS yanogesha mambo ujenzi maabara Dodoma, Mwanza

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button