TRA yataka wafanyabiashara wasiogope kodi

GEITA; MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Geita, imewataka wafanyabishara kufanya biashara zao bila woga wa sheria ya kodi, badala yake wazingatie sheria kwa kulipa kodi kuchangia mapato serikalini.

Ofisa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano TRA Mkoa wa Geita, Justine Katiti amebainisha hayo alipokutana na wafanyabiashara Kata ya Muganza wilayani Chato kuhamasiha kampeni ya Tuwajibike.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dk Samia Suluhu Hassan inatamani kuona kila sekta ikiwemo sekta ya biashara inakua na hivo wafanyabiashara wawe huru na wazingatie sheria za nchi.

Katiti amesisitiza wafanyabiashara hao kuliwekea mkazo suala la kutunza kumbukumbu za biashara zao na kudai risiti za manunuzi, kutoa risiti za Mashine za Kielektorniki (EFD) kwa kila mauzo.

Amesema utunzaji wa gharama wanazotumia kwenye biashara zao inaweka msingi bora wakati wa kufanyiwa makadirio ya kodi, kulipa kodi stahiki na kupunguza migogoro ya kodi na kukuza biashara zao.

Amewakumbusha kuwa madhara ya kutotoa au kudai risiti yanasababisha serikali kupoteza mapato yake na hivyo kurudisha nyuma mipango ya serikali ya kuleta maendeleo kwa wananchi wake.

Katiti amewashauri pia wafanyabiashara kurasimisha biashara zao kwa kufika TRA na kujisajili kwa kupatiwa namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN), ikiwa ni utambulisho wa biashara zao kisheria.

Mwenyekiti wa Kata ya Muganza wilayani Chato, James Mpanduji alikiri kampeni ya Tuwajibike inayoratibiwa na TRA imewaleta pamoja wafanyabisahara, wananchi na serikali kwa ujumla.

Amesema kupitia kampeni hiyo wamekumbushwa wajibu wao kama walipakodi na madhara ya kutofuata sheria za kodi ikiwemo kutotoa risiti za EFD na kuahidi kuendelea kuiunga mkono TRA.

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Julia
Julia
1 month ago

I’m making over $7k a month working component time. I saved hearing other people inform me how lots cash they could make online so I decided to look at it. Well, it turned into all proper and has definitely modified my life.
.
.
Detail Here————————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

Marry
Marry
1 month ago

Surprising! I’ve been making 100 Dollars an hour since I started freelance on the Internet six months ago. I work long hours a day from home and do the basic work that I get from the business I met online. share this work for you opportunity This is definitely the best job I have ever done………


…Go To This Link…………… > > > > http://Www.Smartcareer1.com

Karenray
Karenray
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Karenray
Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x