MAREKANI : RAIS wa zamani wa Marekani Donald Trump amesema hatashiriki mdahalo mwingine na mpinzani wake Kamala Harris. Ingawa kura za maoni zilionyesha kuwa Harris alishinda mdahalo wa kwanza.
“Hakutakuwa na mdahalo wa tatu” alisema Trump mwenye umri wa miaka 78 aliandika kwenye jukwaa lake la Truth Social.”
Trump alitoa msimamo huu baada ya Kamala Harris kurejea kwenye kampeni katika majimbo yenye maamuzi makubwa ya uchaguzi wa Rais wa Marekani
SOMA : Harris na Trump wakutana tena
Kinyang’anyiro hiki cha kutaka kuingia Ikulu ya Whitehouse kitaamuliwa ifikapo Novemba mwaka huu.
SOMA : TRUMP, HARRIS NGOMA NGUMU