TUCTA yaahidi kutetea maslahi ya wafanyakazi

DAR ES SALAAM; Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania – TUCTA) limesema litaendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali katika kusimamia na kutetea haki, maslahi na ustawi wa wanachama wake, kwa lengo la kuhakikisha mazingira bora ya kazi, mishahara stahiki na heshima kwa wafanyakazi nchini vinaimarishwa.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam Februari 25, 2026 na Cde. Saidi Wamba kwa niaba ya Katibu Mkuu wa TUCTA wakati wa ziara ya Mbunge wa Viti Maalum anayewakilisha kundi la Wafanyakazi Mhe. Beng’i Issa  aliyoifanya katika Ofisi za TUCTA.

Cde. Wamba pamoja na mambo mengine amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya vyama vya wafanyakazi na Serikali ni muhimu katika kujenga mahusiano mazuri ya kikazi na kuongeza tija katika maeneo ya kazi.

Amesema TUCTA itaendelea kusimamia masuala ya msingi yanayogusa wafanyakazi, ikiwemo mikataba ya ajira, usalama na afya kazini, pamoja na ustawi wa wafanyakazi katika sekta mbalimbali za umma na binafsi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Masuala ya Jinsia, Vijana, Wenye Ulemavu na Wafanyakazi Wahamiaji Wakili Nasra Shargy ameeleza umuhimu wa kuzingatia usawa wa kijinsia mahali pa kazi, akisisitiza kuwa wafanyakazi wanawake wanapaswa kupewa fursa sawa na kulindwa dhidi ya aina zote za unyanyasaji na ubaguzi.

Naye Mbunge wa Viti Maalum,  Beng’i Issa, amewataka wafanyakazi ambao bado hawajajiunga na vyama vya wafanyakazi kujiunga mara moja, akieleza kuwa uanachama unaleta nguvu ya pamoja katika kutetea haki na maslahi yao.

Amesema kupitia vyama vya wafanyakazi, wafanyakazi hupata fursa ya kusikilizwa, kushirikishwa katika maamuzi yanayowahusu, pamoja na kupata msaada wa kisheria na kitaaluma pale inapobidi.

TUCTA imeeleza kuwa itaendelea kutoa elimu kwa wafanyakazi kuhusu haki zao na wajibu wao, huku ikihimiza mshikamano na uwajibikaji katika maeneo ya kazi kwa maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Habari Zifananazo

4 Comments

  1. Yanga yatuma salamu Msimbazi ikiichapa JKT Tanzania 5-0

    1. I get paid over (90$ to 200$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $18000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
      .
      HERE——————————————⊃⫸ https://Www.Cash54.Com

    2. I get paid over 220 Dollars per hour working from home with 2 kids at home. i never thought i’d be able to do it but my best friend earns over 15k a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life. This is what I do, check it out by Visiting Following Website…

      .
      M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

  2. Yanga yatuma salamu Msimbazi ikiichapa JKT Tanzania 5-0.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button