Tuwekeze kwenye soka la watoto kitaalamu

NDOTO za Taifa Stars kuwa moja kati ya timu nne zitakazopata nafasi ya kucheza mechi za mchujo kuwaniakufuzu fainali za Kombe la Dunia zitakazoandaliwa kwa pamoja na Marekani, Canada na Mexico mwakani, zimekufa.

Ndoto hizo zimeota mbawa baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na timu ya taifa ya Zambia ‘Chipolopolo’ Uwanja wa Amaan Compex, Unguja, Zanzibar Jumatano.

Lakini kukosekana kwa nafasi hiyo kwa Taifa Stars baadhi ya mashabiki wa soka wa Tanzania wanaamini, Kocha Mkuu wa timu hiyo Hemed Suleiman ‘Morocco’ hatoshi kwa nafasi hiyo.

Morocco aliyeongoza Taifa Stars kufuzu fainali zake za tatu za Mataifa ya Afrika zitakazoanza nchini Morocco, Desemba mwaka huu anaonekana hatoshi na kwamba mashabiki hao wanaamini Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapaswa kusaka kocha mwingine atakayeifikisha Tanzania kwenye mafanikio zaidi.

SOMA: NBC, wadau waendesha kliniki ya michezo kwa watoto

Labda pengine ni kumtoa kafara kocha huyo mzawa alieonekana kuaminiwa na TFF huku zikiwekwa kando sababu za msingi zitakazolipeleka soka la Tanzania mbele zaidi na hivyo kuwa na timu ya taifa imara.

Mara kwa mara gazeti hili limekuwa mstari wa mbele kuhubiri juu ya kutengeneza msingi mzuri wa soka la vijana kuanzia umri mdogo kabisa na si kuanzia umri wa miaka 15 ama 17 ikiaminika kwa kufanya hivyo basi Taifa Stars inaweza kupata wachezaji mahiri kwa baadaye.

Kuna kila sababu wadau wote wa soka kuiunga kwa vitendo serikali kwenye juhudi zake za kutaka kuona soka la Tanzania linapiga hatua kubwa kwa kuandaa mazingira bora kwa mchezo huu kuchezwa kwa ufanisi mkubwa.

Serikali imekuwa mstari wa mbele kutengeneza miundombinu rafiki kuhakikisha mchezo huu unaopendwa zaidi duniani ikiwemo ukarabati na ujenzi wa viwanja vya kisasa, unachezwa kwa kiwango cha juu na Taifa Stars inapata mafanikio makubwa.

Umri sahihi wa kuanza kuwekeza ni miaka sita na si miaka 15 au 17 kama ambavyo wachezaji wengi wa Taifa Stars wameanza kuonekana katika umri huo.

Uwekezaji kwenye soka la watoto watakaokwenda ngazi kwa ngazi unahitaji dhamira ya dhati kwa wale wote wenye mapenzi na mchezo huu wa soka ikiwemo kuajiri walimu wajuzi wa soka la umri mdogo kutoka nchi zinazosifika kwenye kuendeleza soka la vijana kama Hispania, England, Ufaransa, Ubelgiji na nyinginezo katika bara la Ulaya.

Uwekezaji unaofanywa na serikali kwenye miundombinu ya mchezo huu karibu kila kona ya nchi unapaswa kuungwa mkono na wadau wake kwa kuanza kutengeneza kitaalamu soka la watoto ambao baadaye watakuja kucheza timu za ngazi mbalimbali za vijana na mwisho Taifa Stars.

Siku mtego huu ukiteguliwa basi Tanzania itakuwa moja ya mataifa tishio katika mchezo wa soka duniani lakini kwa kuruka hatua kama ilivyo sasa basi kila kocha wa Taifa Stars atajikuta kwenye lawama.

Habari Zifananazo

4 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. I­ g­­­­­e­t­­­­ p­a­i­­­d­­­­­­­ o­­­­­v­e­r­ 2­­­2­­­0­­­ D­­­o­­­­­­lla­­­r­­­­­s p­­­­­e­­­­­r­ ­­­h­o­­­­­u­r­­­ ­­­­w­­­­o­r­k­­i­­­­n­g­ f­r­o­­m­ h­o­m­e­ ­w­i­t­h­­ 2 k­i­d­­s­ a­t­ h­o­­m­e­. i­ n­e­v­e­r­ t­h­o­u­g­h­t­ i­’d­ b­e­ a­b­l­e­ t­o­ d­o­ i­t­ b­u­t­ m­y­ b­e­s­t­ f­r­i­e­­n­d­ e­a­r­­n­s­ o­v­­e­r­ 1­5k­ a­ m­­o­n­t­h­ d­­o­i­n­g­ t­h­­i­s­ a­n­d­ s­­h­e­ c­o­n­v­i­n­c­­e­d­ m­e­ t­o­ t­r­­y­. it was all true and has totally ch­a­n­g­e­d­ ­m­y­ l­i­f­e­. T­h­i­s­­ ­i­s­ ­w­h­a­t­­ ­I­ ­d­­o­­­­­­­,­­­­­­­ ­c­h­­­­­e­­­­c­­­­k­ ­­­­i­­­­t­ ­o­­­­­u­t­ ­­­­b­y­ ­­­­V­i­s­­­­­i­t­i­n­­­­g ­F­o­­­­l­l­o­w­i­­n­­­­­g ­W­e­b­s­­­­­i­t­e

    ­
    Open This…. https://Www.Work99.site

  4. Google pays $220 an hour online. My close relative had been unemployed for nine months, but last month, she received a $25k paycheck by working from home for 10 hours a day. Everyone should try this job now—just use this link. COPY THIS →→→→ https://Www.Salary7.Zone

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button