UFAWAZA wampa kongole Mavunde
UMOJA wa familia ya wanamichezo wa zamani Dodoma(UFAWAZA) wametoa shukrani zao kwa Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde kwa udhamini wa Huduma ya Bima ya ‘NISHIKE MKONO’ inayotolewa na Benki ya Biashara Tanzania (TCB).
Akitoa salamu hizo Mwenyekiti wa UFAWAZA, Ally Kheri amemshukuru Mbunge Mavunde kwa kuwa karibu na kuusaidia umoja huo tangu kuanzishwa kwake Novemba 27, 2021 ikiwa ni pamoja na udhamini wa bima ambao umegharimu Sh milioni 3.6 kwa wanachama 75 .
Bima ya Nishike Mkono mwanachama ambae anapata tatizo la kufiwa upatiwa kiasi cha sh milioni 1.2
Akipokea shukrani hizo, Mavunde ameshukuru UFAWAZA kwa kutambua mchango wake na kuahidi kuendelea kushirikiano nao katika kuinua michezo Jijini Dodoma.
“Ninawashukuru kwa kutambua mchango wangu kwenye umoja wenu huu na nitaendelea kuwa nanyi bega kwa bega; ….. “Dodoma tumejipanga vizuri kuwapa heshima na kutambua mchango wa wanamichezo wa zamani.”Amesema
Mavunde, amesema, pamoja na Bima hiyo ya NISHIKE MKONO, hatua inayofuata ni kuhakikisha wanapata uhakika wa Bima ya Afya ambapo kwa mujibu wa taratibu lazima wafikieshe idadi ya wanachama 100 ndio waingie kwenye mfuko wa Umoja Afya wa Bima ya Taifa.
“Tukikamilisha takwa hilo la usajili nitawachangia Sh milioni 5 kwa ajili ya malipo ya mfuko wa Umoja Afya.” Amesema Mavunde