Upungufu wa maji kuongezeka

MAREKANI : TUME ya Kimataifa ya Uchumi wa Maji- GCEW, imesema tatizo la upatikanaji wa maji litaongezeka na kitasababisha nusu ya uzalishaji wa chakula duniani kuwa hatarini 2050.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa hivi karibuni imeonesha takriban watu bilioni 3 wako katika maeneo ambayo hifadhi ya maji inapungua.

Pia imeonesha tatizo  la maji litasababisha  kushuka kwa asilimia nane ya Pato la Taifa kwa wastani katika nchi zenye kipato cha juu ifikapo mwaka 2050 na hadi asilimia 15 kwa nchi zenye kipato cha chini. Ingawa maji mara nyingi huchukuliwa kama rasilimali asili.

Advertisement

Kufuati tatizo hili wadau wa maji wameelekezwa kuanza  kuchukua hatua ili kudhibiti  upungufu wa maji unaotegemewa katika uzalishaji wa chakula.

SOMA: Mradi wa maji Ruvu kukamilika 2025