Upelelezi kesi ya Hussein Hariri wakamilika

UPANDE wa mashitaka katika kesi  ya tuhuma za kusafirisha kilogramu 1001.

17 za dawa za kulevya aina ya heroin inayomkabili mkazi wa Mikocheni, Dar es Salaam, Hussein Hariri na wenzake wawili  umedai upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Wakili wa Serikali Caroline Matemu alidai  hayo leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Mery Mrio.

Advertisement

Matemu alidai mahakamani hapo kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi umekamilika na wanasubiri kuwasilisha taarifa Mahakama Kuu na aliiomba mahakama kupanga tarehe nyingine, ili washitakiwa waweze kusomewa maelezo ya ushahidi.

Hakimu Mrio aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 16, mwaka huu na washitakiwa wataendelea kubaki rumande.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Benson Muro (32) mkazi wa mbezi na Ramadhani Almas (46) mkazi wa magomeni mapipa.

Katika kesi hiyo inadaiwa kuwa  washitakiwa hao walitenda kosa hilo Machi 17 mwaka jana eneo la Mbezi Chini.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *