Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere mambo mazuri

DAR ES SALAAM: SERIKALI imetoa wito kwa mashirika ya ndege ya ndani na nje ya Tanzania kutumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kwani ulinzi na usalama kwa ndege, abiria na mizigo umeendelea kuimarishwa kwa kuweka mifumo ya kisasa.

Akizungumza mara baada ya kukagua miundombinu ya jengo la tatu la abiria katika kiwanja hicho jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri David Kihenzile amesema uwepo wa usalama umeendelea kuwa na matokeo chanya kwani idadi ya mashirika yanayohudumiwa yamekuwa yakiongezeka ikiwemo Shirika la Ndege la Ufaransa na Shirika la Ndege la Saudia.

“Serikali inayongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kwa dhati kuhakikisha miundombinu ya viwanja inaboresha na mashirika yanayongezeka kwenye viwanja vyetu,” amesema Kihenzile.

Amesema hivi karibuni wameongeza mashirika mawili ya nje na moja la ndani kutoa huduma kupitia kiwanja hicho na kwamba hiyo ni hatua kubwa.

Kihenzile ameipongeza TAA kwa kuendelea kusimamia viwanja vya ndege na kuhakikisha hatua za haraka zinachukuliwa inapotokea changamoto za kiuendeshaji hali inayoongeza imani kwa abiria na mashirika ya ndege.

Amesema mipango ya serikali ni pamoja na kulifanyia ukarabati mkubwa jengo la pili la abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, ambapo litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria zaidi ya milioni 3, badala ya milioni 1.5 waliokuwa wakihudumiwa kwa mwaka.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TAA Mussa Mbura, amesema mamlaka yake imejipanga kuhakikisha inaboresha zaidi viwanja vya ndege nchini ili kukuza utalii na kuongeza pato la nchi.

Naye Mkurugenzi wa JNIA, Mhandisi Rehema Myeya amesema kwa sasa jengo hilo la tatu la abiria linafanya kazi kwa saa 24 na abiria zaidi ya 2000 wanaweza kuhudumiwa kwa wakati mmoja.

Kihenzile yuko katika ziara ya siku tano jijini Dar es Salaam ya kukagua miundombinu ya uchukuzi.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Work AT Home
Work AT Home
1 month ago

Earn money in USA, high scores from trusted resources. Work at your own pace. Regular Payments. Search in different job categories. Work anywhere on your vs03 computer, laptop or mobile phone. Update your profile at any time.
.
.
Detail Here———->>> http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work AT Home
FloellaRainbow
FloellaRainbow
1 month ago

★My buddy’s mother makes $90 per hour working on the computer (Personal Computer). She hasn’t had a job for a long, ( w99q) yet this month she earned $15,500 by working just on her computer for 9 hours every day.
Click and Copy Here══════►►► http://Www.SmartCareer1.com

Angles
Angles
1 month ago

Google pay 390$ reliably my last paycheck was $55000 working 10 hours out of consistently on the web. (0w)My increasingly youthful kinfolk mate has been averaging 20k all through continuous months and he works around 24 hours reliably. I can’t trust how direct it was once I attempted it out. This is my essential concern…:) GOOD LUCK
For more info visit………….. http://www.Smartcash1.com

Julia
Julia
1 month ago

I’m being paid 185 dollars per hour to work on my home computer. I had no clue it was possible, but a close friend made $25,000 in four weeks by completing one outstanding job, and she persuaded me to join.
.
.
Detail Here——————————————————>>>  http://Www.BizWork1.Com

Nancynglin
Nancynglin
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Nancynglin
Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x