Wanafunzi Morogoro, Dodoma kupewa elimu stadi za maisha

WANAFUNZI wa shule za sekondari  kutoka Halmashauri za  Wilaya ya Malinyi na Manispaa ya Morogoro  mkoani  Morogoro pamoja na Chamwino, Dodoma wanatarajia kupatiwa elimu ya  stadi za maisha  kupitia mradi  utakelezwa na Shirika lisilo la kiserikali la Campaig For Female Educations (CAMFED).

Mradi huo unatarajia kutekelezwa mwaka wa masomo  2024 na unalenga kutatua changamoto  mbalimbali za wanafunzi, kuthibiti mdondoko shuleni , kutojitambua na kuwaepusha  kujiingiza kwenye vishawishi viovu.

Meneja Miradi wa Camfed, Latifa Sabuni amesema hayo  mjini Morogoro wakati kikao kazi cha utoaji wa elimu kwa wakuu wa shule za sekondari 29 za Manispaa ya Morogoro na kuutambulisha mradi huo utakaotekelezwa katika  halmashauri ya  Manispaa ya Morogoro, Malinyi  na Chamwino .

Shirika la Camfed limeazishwa  mwaka 2005 na kusajiliwa  mwaka 2006  na kwa sasa  linafanya kazi  kwenye mikoa 10 nchini  katika  wilaya 33.

Sabuni amesema, kwa sasa mradi wa ‘Life skills’ ni mpya kwenye  shule hizo na haukuwahi kuwemo  katika  mradi unaofanyika   na Shirika hilo .

Amesema wanafunzi hao watapewa stadi za maisha  zitakazo wasaidia kujitambua  na kujithamini  kwa lengo la kupata elimu yao bila ya vikwanzo.

Sabuni amesema ni mradi wa kujitolea ambao  utawatumia vijana waliohitimu shule ili kusaidia wenzao    waweze  kuendelea kubaki shuleni  na kuchangia ufaulu uongezeka  zaidi.

“Program hii itaanza  Januari 2024, tupo  kwenye maandalizi ya awali ya uchaguzi  wa hao vijana , namna ya kuwafanyia mafunzo, lengo ni kuanza na wanafunzi wa kidato cha kwanza wanaoanza mwaka wa masomo 2024” amesema Sabuni

Sabuni amesema mradi huo upo kwa ajili ya kulisaidia taifa letu katika kuwawezesha wanafunzi kujitambua watambue umuhimu wao wa kukaa shule , kuendelea na masomo na sio kuishia njiani kidato cha pili .

Naye mshauri wa Camfed na Mhadhiri Mwandamizi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Dk Siafu Sempeho amesema lengo ni kuhakikisha wanafunzi wenye dalili za kudondoka kutoka kwenye mfumo rasmi wa shule wanaweza kutambuliwa mapema  na kusaidiwa ili kupunguza mdondoko.

Dk Sempeho amesema , watateuliwa wanafunzi waliomaliza shule na kupewa mafunzo  ya namna bora ya kuwaongoza wenzao kwa kutambua viashiria vya mdondoko wa mapema .

Vijana hao watashirikiana na walimu wa unasihi shuleni  na waongozaji wa wanafunzi  ili  mradi huo uweze kusaidia  mzunguko wa elimu  kuona wanafunzi wanaendelea kutoka darasa la saba hadi kidato cha kwanza , cha pili , nne na  kidato cha tano  bila  kukwama njiani.

Dk Sempeho amesema  ,kutakuwa na vikundi vya wazazi vitaundwa vikiwa na lengo la kuifanya jamii yenyewe ione inawajibika kusaidia watoto wao wabaki shuleni kwa kushirikiana na walimu na kufanya ubora wa elimu kuwa juu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa wakuu wa shule za sekondari Manispaa ya Morogoro, Festo Kayombo amesema wataandaa vipindi darasani na kuweka kwenye ratiba ya masomo la elimu stadi za maisha  kwa wanafunzi ili kuwakinga  na vihatasishi vinavyowazunguka wakiwemo bodaboda .

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
AngliaSteve
AngliaSteve
1 month ago

Working part-time and making an extra $15,000 or more online is a simple and quick method to gain money. I made $17,000 in the previous month by working in my spare time, and I am really satisfied now as a result of this job. 
.
.
Detail Here——————————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

MAPESA1234567
MAPESA1234567
1 month ago

HE/SHE DIED WITH CARDINAL RUGAMBWA HOSPITAL DISEASE… THE HISTORY OF THIS DISEASE WAS KILLED MORE THAN 5 MILION PEOPLE AROUND THE WORLD MANY WAS CHINESE, EROPEAN, KOREAN AND INDIANS… ALL WHERE WHITE SKIN PEOPLE

MAPESA1234567
MAPESA1234567
1 month ago

HE/SHE DIED WITH CARDINAL RUGAMBWA HOSPITAL “CONFERENCE” DISEASE… THE HISTORY OF THIS DISEASE WAS KILLED MORE THAN 5 MILION PEOPLE AROUND THE WORLD MANY WAS CHINESE, EROPEAN, KOREAN AND INDIANS… ALL WHERE WHITE SKIN PEOPLE…. KILICHOBAKI BABA/BWANA YESU ASIFIWE DISEASE

MONEY
MONEY
1 month ago

KWELI WEWE JAMAA KWAKO HAKUNA BAG

TUNZA MAZINGIRA YAKUTUZE… UTAKACHOONDOA NDIO KAZI..

100% KIWEKWACHO HUMO HUTENGENEZWA NA WANAWAKE

file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg

file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image004.jpg

Capture.JPG
Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x