Wanawake kupatiwa matiti bandia Muhimbili

WANAWAKE wanaokumbwa na changamoto ya kuondolewa matiti kufuatia ugonjwa wa Saratani ya Matiti sasa wanatarajiwa kunufaika na msaada wa matiti bandi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Akizungumza wakati wa kupokea msaada huo jijini Dar es Salaam, kwa niaba ya MNH, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba, Dk Faraja Chiwanga, amesema msaada huo ni muhimu kwa wagonjwa kwani utawasaidia kurejesha hali yao ya kujiamini baada ya kufanyiwa matibabu.

“Tunatoa pongezi za dhati kwa Umoja Pharmaceuticals kwa moyo wao wa kujali. Wagonjwa wa saratani ya matiti hupitia changamoto kubwa si tu kimwili bali pia kisaikolojia, hivyo msaada huu utasaidia kuwapa faraja na kuimarisha hali yao ya maisha,” amesema.

Ameongeza kuwa hospitali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma bora na msaada unaohitajika katika kila hatua ya matibabu yao. SOMA: MOI kufanya upasuaji wa saratani ya ubongo

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja Pharmaceuticals, Lucy Lushiku, amesema kampuni hiyo imeguswa na changamoto wanazokutana nazo wagonjwa wa saratani ya matiti, hususan baada ya kufanyiwa upasuaji, na hivyo kuona umuhimu wa kuwasaidia wanawake hao. “Sisi tunaamini kuwa afya si matibabu ya mwili pekee, bali pia ustawi wa kisaikolojia. Ndiyo maana tumeamua kutoa msaada huu ili kuwasaidia wanawake hawa kurejesha tabasamu lao,” amesema.

Hospitali ya Taifa ya Muhimbili inaendelea kutoa huduma mbalimbali za kibingwa ikiwemo matibabu ya saratani ya matiti, huku ikijikita katika huduma jumuishi zinazohusisha matibabu, ushauri nasaha na ufuatiliaji wa wagonjwa baada ya matibabu.Msaada huo umetolewa na Umoja Pharmaceuticals wenye thamani ya shilingi milioni 400 ukiwa na lengo la kuboresha hali za kisaikolojia na maisha ya wanawake hao baada ya matibabu.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. I get paid over 220 Dollars per hour working from home with 2 kids at home. i never thought i’d be able to do it but my best friend earns over 15k a month doing this and she kaz convinced me to try. it was all true and has totally changed my life. This is what I do, check it out by Visiting Following Website

    HERE————— w­­w­­w­­.­­w­­o­­r­­k­­2­­7­­.­­o­­n­­l­­i­­n­­e

  2. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  3. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button