Waziri Mkuu azindua mpango mkakati wa amref

Asisitiza mashirika yasiyo ya kiserikali kuzingatia maadili

DAR ES SALAAM: Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amezindua Mpango Mkakati wa miaka nane wa AMREF Tanzania na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kufanya ufuatiliaji ili kuhakikisha afua zilizopo katika mpango huo zinatekelezwa kwa ufanisi na kuboresha huduma za afya kwa Watanzania.

Majaliwa amesema kuwa mpango mkakati huo ambao unatarajia kugharimu dola za kimarekani milioni 458 kwa miaka yote nane utajikita katika kuboresha Afya ya msingi ikiwemo, kutekeleza afua za afya ya uzazi pamoja na afya ya mama na mtoto, afua za magonjwa yasiyoambukiza utasaidia katika kuimarisha afya na ustawi wa Watanzania

Ameyasema hayo, Septemba 15, 2023 wakati akizindua mpango huo katika Hoteli ya Serena, Dar Es Salaam. Mpango mkakati huo kuanzia mwaka 2023 hadi 2030 ili kuelekea katika malengo ya maendeleo endelevu ya dunia 2030.

“Niwahakikishie kuwa, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Afya Tanzania Bara, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Wizara ya Afya Zanzibar, na wizara nyingine zote ambazo shughuli zenu zinahusiana nazo itaendelea kushirikiana na Amref Tanzania katika utekelezaji wa mpango mkakati huu”

Katika Hatua nyingine Majaliwa ametoa wito kwa Mashirika yasiyo ya Kiserikali, kuzingatia maadili ya nchi wakati wa utekelezaji wa afua mbalimbali.

“Msikubali kutumika kuwa chombo cha kuhamasisha mmomonyoko wa maadili ya Taifa letu. Kila shirika litekeleze majukumu yake kwa kuzingatia mkataba uliopo kati yake na Serikali. ”

Aidha, amezitaka Mamlaka zote za Serikali zinazohusika na usajili wa mashirika yasiyo ya Kiserikali kufuatilia kwa karibu utendaji wa mashirika hayo ili kuzuia mianya ya kuhamasisha vitendo vya mmonyoko wa maadili.

Naye Mkurugenzi Mkazi wa AMREF Tanzania Dkt. Florence Temu amesema gharama za kutekeleza mpango mkakati huo itakuwa inaongezeka mwaka hadi mwaka ambapo kwa mwaka 2023 itakuwa ni Dola za marekani milioni 40 ambayo itakuwa ikikua kwa asilimia 30.

 

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Ashleyngram
Ashleyngram
17 days ago

I am now making more than 350https://s.w.org/images/core/emoji/14.0.0/svg/1f4b0.svg dollars per day by working online from home without investing any money.Join this link posting job now and start earning without investing or selling anything……. 
🙂 AND GOOD LUCK.:)..____ http://Www.Careers12.com

Last edited 17 days ago by Ashleyngram
Beth Rector
Beth Rector
Reply to  Ashleyngram
17 days ago

I have a home-based business and make a respectable $60k per week, which is incredible given that a year ago I was unemployed due to a poor economy. I was given these instructions as a gift, and it is now my ne-02 responsibility to spread kindness and make them available to everyone.
.
.
This Page Provides Details—————>>> http://bigmoney8.store

MONEY@
MONEY@
14 days ago

PATA DOLLA $45,000,000 SASA FANYA KAZI NYUMBANI NA HUTAKIWI KUTOKA HATA KIDOGO KABISA

TANGAzo

Chama cha MAPINDUZI kinawatangazia VIJANA WA KITANZANIA 500,000 kuandaa kijiji cha ujamaa eneo la UVUMI DODOMA…

WAHI FURSA HII ADIMU KWA MAENDELEO YA KARNE YA 23

Capture.JPG
Bima Ninayo
Bima Ninayo
14 days ago

IKASAIDIE KUONGEZA NGUVU ZA KIUME KWENYE VIJIJI VYA UJAMAA 

CaptureA.JPG
Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x