Waziri mkuu mpya ajiuzulu Ufaransa

PARIS: WAZIRI Mkuu wa Ufaransa, Sebastien Lecornu, aliyeteuliwa hivi karibuni, amejiuzulu Jumatatu katika hatua ambayo haikutarajiwa. Ikulu ya Elysée imesema barua ya kujiuzulu ya Lecornu imewasilishwa kwa Rais Emmanuel Macron, ambaye ameikubali bila kuchelewesha.

Hatua hiyo imejiri saa chache tu baada ya Lecornu kuteua baraza lake jipya la mawaziri, ambapo nafasi nyingi muhimu ziliendelea kushikiliwa na mawaziri waliokuwepo awali. Wakati huo huo, upinzani wa kisiasa nchini Ufaransa ulikuwa umetishia kuangusha serikali yake, jambo linaloashiria mzozo mkubwa wa kisiasa na mkwamo unaoendelea nchini humo.

Siasa za Ufaransa ziliingia kwenye misukosuko baada ya Rais Macron kuapishwa kwa muhula wa pili mwaka 2022, na kuongezeka zaidi baada ya uchaguzi wa mapema wa Bunge mwaka jana, ambapo hakuna chama chochote kilichofanikiwa kupata wingi unaohitajika wa wabunge.

Hali hiyo inaashiria changamoto kubwa kwa serikali ya Rais Macron katika kusimamia sera zake, huku ukosefu wa wingi wa wabunge ukikwamisha utekelezaji wa miradi na mipango ya kisiasa. SOMA : Macron amteua Lecornu Waziri Mkuu mpya

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button