Wasifu uwepo wa jengo la watoto njiti Kwimba

MWANZA; Wanawake wawili wa wilayani Kwimba, mkoani Mwanza wamezungumzia changamoto walizopitia wakati wa kujifungua, wakilazimika kusafiri umbali mrefu kwa pikipiki wakiwa na uchungu hadi hospitalini na kujifungua watoto njiti.

Happyness Muhaji, amesema alisafiri kwa zaidi ya saa mbili na mtoto wake hakulia hadi baada ya saa nane, kisha alikaa wiki moja bila kumuona kutokana na uangalizi maalumu.

Amemshukuru Doris Mollel Foundation (DMF) kwa kuwajengea jengo la kisasa la huduma za watoto njiti lililosogeza huduma karibu na kusaidia kina mama wengi. Hata hivyo, amelalamikia ukosefu wa ushirikiano kutoka kwa baba wa mtoto ambaye humpa shilingi elfu 10 tu kwa matumizi ya mwezi.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Dk. Fredrick Mugarula, amesema ujio wa DMF chini ya Mkurugenzi wake Doris Mollel umesaidia kupunguza vifo vya watoto wachanga.

Mwaka 2025, wilaya hiyo ilirekodi watoto 24,241 waliozaliwa, 146 wakifariki ndani ya siku 28, huku 1,640 wakiwa njiti. Ujenzi wa jengo jipya la wodi ya watoto wachanga na nyumba za wauguzi vya watoto wachanga.

Mwaka 2025, wilaya hiyo ilirekodi watoto 24,241 waliozaliwa, 146 wakifariki ndani ya siku 28, huku 1,640 wakiwa njiti. Ujenzi wa jengo jipya la wodi ya watoto wachanga na nyumba za wauguzi

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button