Jaji Chande azungumzia safari ya utendaji wa tume
DAR ES SALAAM: MWENYEKITI wa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Oktoba 29, Jaji Mkuu mstaafu, Mohamed Chande, amezungumzia tume itamaliza kazi Aprili 24 na kutoongezewa tena muda, alijibu ndilo lengo kwa kuwa safari imefikia ukingoni.
Akizumgumza Dar es Salaam, Jaji Chande alisema kazi kubwa iliyobaki ni kuendelea kupokea na kuchambua ushahidi wa mwisho, uandishi wa ripoti kwa lugha ya Kiswahili na Kingereza na kusisitiza; wanatambua kina, ukubwa, uzito na umuhimu wa kazi hiyo.
Jaji Chande alisisitiza, “Tuko karibu mno na mwisho wa safari. Tulianza bila wafanyakazi sasa tunakaribia mwisho wa safari.”



