Kigoma yatarajia kuuza kilo milioni 15 za tumbaku

KIGOMA: Zaidi ya kilo milioni 15 za tumbaku zinatarajiwa kuuzwa na wakulima kwa kampuni za ununuzi wa zao hilo mkoani Kigoma kwa msimu huu wa kilimo.

Kaimu Meneja wa Kanda ya Magharibi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB), Elisha Chao, amesema hayo akiwasilisha taarifa ya bodi hiyo kwa wajumbe wa kikao cha wadau wa kahawa mkoa Kigoma kilichofanyika mjini Kigoma jana.

Chao amesema hadi sasa kilo milioni 15 zimenunuliwa na bado kuna tumbaku ipo sokoni na wanunuzi wanaendelea na taratibu za ununuzi kwenye masoko hayo.

Amesema mwaka huu kumekuwa na ongezeko kubwa la uzalishaji kutokana na soko lililokuwepo msimu uliopita na bei iliyokuwepo na kwamba TTB inasimamia kwa karibu kuhakikisha tumbaku iliyiozalishwa inaunuliwa yote.

Akizungumza katika mkutano huo Mkoa wa Kigoma Balozi ,Simon Sirro, ametaka wadau wa zao la tumbaku nchini kusimamia taratibu za kilimo na uuzaji wa zao hilo ili kuhakikisha mkulima ananufaika na kuwa na maendeleo.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma amesema uzalishaji wa zao la tumbaku mkoani humo umeendelea kuongezeka, kutoka tani 4,452 mwaka 2021/2022 hadi tani 14,213 mwaka 2024/2025.

Amesema ongezeko hilo la uzalishaji limechochea pia kuongezeka kwa mapato ya Serikali, kutoka Sh bilioni 15.4 mwaka 2023/2024 hadi Sh bilioni 26.9 mwaka 2025/2026.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button