EAC, SADC msikate tamaa amani DRC

HIVI karibu askari wawili wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania (JWTZ) walipoteza maisha katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda aliwasilisha salamu za rambirambi na ubani kwa familia ya askari waliopoteza maisha wakilinda amani nchini humo.

Walikuwa DRC ambayo ni mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kushiriki ulinzi wa amani.

Walipoteza maisha kutokana na mapigano baina ya kikundi chao na kundi la M23.

Kimsingi, ni utaratibu wa Tanzania kupeleka askari wake katika nchi ambazo amani inatetereka na wanakwenda chini ya mwavuli wa ama Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) au EAC.

Askari wengine wapo katika nchi za Lebanon, Afrika ya Kati, Msumbiji na Congo. Tunalipongeza JWTZ kwa ujasiri na uzalendo wake kwa Afrika na kuendelea kuhakikisha linatoa mchango wa hali na mali kulinda na kudumisha amani miongoni mwa nchi za Afrika.

Hii inatukumbusha ukweli kuwa, ‘binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.’

Kadhalika, tunazipongeza nchi zote zinazojitoa kupeleka askari wake kusaidia ndugu zetu katika nchi zenye tabu kwa kuwa nyingine licha ya kuwa na changamoto kukosa amani, pia zinateswa na athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi na magonjwa mbalimbali.

Tunaamini kuwa, changamoto iliyotokea kwa askari hao si tu kwao pekee, bali huwafika hata wengine miongoni mwa
nchi hizo zinazojali udugu.

Wakati Watanzania, wanaEAC na watu wa nchi za SADC wakizidi kuwaombea kila la heri, tunawapa moyo JWTZ katu isikate wala kukatishwa tamaa kwa hatua hii njema wanayofanya.

Aidha, tunahimiza watu wa nchi zenye changamoto ya amani kulinganisha faida na hasara waipatayo kwa ‘kumwagiana damu’ eti kwa sababu tu ya madaraka ambayo katika hali ya kawaida, uongozi na madaraka hutoka kwa Mungu.

Umefika wakati kila upande unaohusika, kunuia kwa dhati kukomesha uhasama huo baina ya ndugu na ndugu,
huku wakizingatia kuwa wapo baadhi ya watu au mataifa wanaoshangilia maana wanajua ‘vita ya panzi ni furaha kwa
kunguru.’

Hao wanapenda uhasama huo uendelee ili ama wazidi kuuza silaha au kuhujumu rasilimali za nchi kwa kujinufaisha wao.

Kadhalika, viongozi na wakuu wa nchi hizo, EAC, SADC na Afrika kwa ujumla wazidi ‘kukuna vichwa’ wakimwomba
Mungu wapate ufumbuzi wa migogoro hii ambayo pamoja na kwamba ipo kwenye nchi hizo, lakini inaathiri ukanda na Afrika kwa ujumla.

Ndio maana tunasema EAC, SADC msikate tamaa kuhusu suala la amani DRC maana Mungu yupo pamoja nanyi.

Habari Zifananazo

7 Comments

  1. Superb website you have here but I was curious if you knew of any community forums
    that cover the same topics talked about in this
    article? I’d really love to be a part of online community where I can get feed-back
    from other knowledgeable people that share the same interest.
    If you have any suggestions, please let me know.
    Thank you!

    My blog post :: BRAND NEW PORN SITE SEX

  2. Viagra has been on the market for many years and the
    blue pill has revolutionized the way in which erectile
    dysfunction is treated. It, however, is connected to a number of unpleasant, even dangerous side effects.

  3. You can get all types of best ED treatments on the official site
    of kamagrauk365 they have the best treatments for male and female sexual problems.

    They also provide coupon discounts and next-day delivery.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button