Madereva bodaboda thaminini kazi yenu

USAFIRI wa pikipiki maarufu kama bodaboda ni moja ya usafi ri unaotegemewa na kutumika sana mikoa mingi hapa nchini.
Pamoja na umuhimu wake baadhi ya madereva wanaotoa huduma hiyo wamegeuka kuwa kero ama kwa abiria au kwa watu wengine wasiotumia huduma hiyo.
Moja ya kero ni tabia ya baadhi ya madereva hao kuweka milio kama bomu kwenye vyombo vyao na kusababisha kushtua watu na wengine kufunga na kufungulia redio kwa sauti kubwa huku akiwa amebeba abiria au kupita mitaani na kusababisha kelele.
Kutokana na kero hizo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenani Kihongosi ametoa siku tatu kwa madereva wa vyombo hivyo kuondoa milio hiyo kama bomu waliyofunga kwenye pikipiki zao, kwa kile alichoeleza kusababisha kelele za kushtua na kusababisha kero kwa wananchi pamoja na watumiaji wa usafiri huo.
Kwa mujibu wa Kihongosi amepokea malalamiko kutoka kwa watu na kuwataka wakumbuke wanapopiga fataki hizo wanasababisha kero kubwa kwa watu wanaosikia, kuna wagonjwa, kuna wazee na wengine wenye shida nyingine na kuwataka wafanye utaratibu wa kuondoa kifaa hicho kinachotoa kelele ndani ya siku tatu.
Tunamuunga mkono mkuu huyo wa mkoa wa Arusha kwa uamuzi huo wa busara kwani vitendo hivyo vimekuwa kero sana kwa wananchi na watumaji wa usafiri huo.
Kama haitoshi baadhi yao wamekuwa wakiambiwa na abiria wanakuwa wakali ama kujibu majibu yasiyofaa kwa abiria na mara nyingine kuwatishia washuke.
Sisi tunaamini kazi ya bodaboda ni kazi kama kazi nyingine na hivyo tunawashauri madereva waheshimu na kuithamini kazi hiyo na kuhakikisha wanaendesha vyombo hivyo vya moto kwa kuzingatia sheria na taratibu.
Tunawasihi watumie kazi yao kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii, watumie fedha vizuri kwa kuwa na malengo ya kimaendeleo.
Tunawakumbusha pia katika kuheshimu na kuthamini kazi zao, muonekano unahusika, kwani baadhi yao wamekuwa wakijiweka kwenye muonekano usioeleweka.
Muonekano ni moja ya vigezo muhimu katika kuvutia biashara, sasa kama dereva bodaboda muonekano wake hovyo, pikipiki kelele sidhani kama abiria anayejielewa anaweza kukodi mtu kama huyo.
Hivyo basi, tunawasihi madereva bodaboda kuifanya biashara hii ya usafiri kuwa ya thamani kuanzia muonekano, lakini pia kikubwa ni kuhakikisha abiria anafika mahali au sehemu anayokwenda kwa amani na usalama.
Kuna baadhi ya abiria wana bodaboda maalumu, kwa sababu tu dereva wa bodaboda hiyo anajiheshimu, anajithamini na makini katika kazi yake.
Aidha, tunaendelea kuwakumbusha madereva wote wa vyombo vya moto kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za barabarani ili kuepuka kukarahisha abiria na wananchi wengine, lakini pia tunawakumbusha kujiheshimu na kuheshimu wengine ili kujiongezea thamani.
I started using this remote work platform about a month ago, and honestly, I was surprised how simple it is. I’m now making 1170+ per week — just from my phone. No special skills, no interviews. If you’re looking for something real and flexible, I’ve shared all the info on my site.
HERE☛ rb.gy/uvl61
I started using this remote work platform about a month ago, and honestly, I was surprised how simple it is. I’m now making 1170+ per week — just from my phone. No special skills, no interviews. If you’re looking for something real and flexible, I’ve shared all the info on my site.
HERE☛?>>>>> rb.gy/uvl61
Gᴏᴏɢʟᴇ ʜᴀꜱ ʙᴇᴇɴ ᴀɴ ɪɴᴄʀᴇᴅɪʙʟᴇ ᴏᴘᴘᴏʀᴛᴜɴɪᴛʏ! ᴇᴀʀɴ 𝟣𝟪𝟢𝟢+ ʙᴜᴄᴋꜱ ᴡᴇᴇᴋʟʏ ꜰʀᴏᴍ ʜᴏᴍᴇ! ᴀ ꜰᴇᴡ ᴍᴏɴᴛʜꜱ ᴀɢᴏ, ɪ ᴡᴀꜱ ꜱᴛᴜᴄᴋ ɪɴ ᴀ ʀᴏᴜᴛɪɴᴇ, ʙᴀʀᴇʟʏ ᴍᴀᴋɪɴɢ ᴇɴᴅꜱ ᴍᴇᴇᴛ. ɴᴏᴡ, ɪ ᴇᴀʀɴ 𝟤𝟢𝟧+ ᴀ ᴅᴀʏ ᴡᴏʀᴋɪɴɢ ꜰʀᴏᴍ ʜᴏᴍᴇ ᴡɪᴛʜ ᴄᴏᴍᴘʟᴇᴛᴇ ꜰʟᴇxɪʙɪʟɪᴛʏ! ɴᴏ ᴇxᴘᴇʀɪᴇɴᴄᴇ? ɴᴏ ᴘʀᴏʙʟᴇᴍ.
ᴊᴏɪɴ ɴᴏᴡ➤➤ http://www.get.money63.com