Magembe ambwaga Kalemani Chato Kaskazini

GEITA: CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chato mkoani Geita kimemtangaza Cornel Magembe kuwa mshindi wa kura za maoni kwa kupata kura 4, 298 katika mbio za kupata mgombea ubunge jimbo la Chato Kasikazini.
Magembe ambaye aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Geita amefuatiwa na aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Chato Dkt Medard Kalemani ambaye amepata kura 1390
Baada ya kutangaza matokeo hayo katibu wa CCM wilayani Chato, Dotto Mazuri amewataka wanachama wa chama hicho kuvunja makundi na kuwa kitu kimoja kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 2025.


