Mgombea urais CUF: Pigeni kura, msisuse

TANGA: Mgombea urais wa Chama cha Wananchi (CUF), Gombo Semandito Gombo amewataka watanzania kutosusia uchaguzi mkuu kwani mabadiliko ya kweli yanatokana katika sanduku la kura.
Kauli hiyo ameitoa wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari mkoani Tanga kuhusu tathimini ya awamu ya kwanza ya kampeni za ugombea urais,ubunge na udiwani
Amesema ni muhimu wapuuzie watu ambao wanafanya ushawishi wa kususia uchaguzi na kufanya maandamano ambayo yatasababisha kuvuruga amani iliyopo.
“Niwaombe watanzania jitokezeni kushiriki kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 29 mwaka huu kama kweli mnataka kuiondoa CCM madarakani kwa njia ya amàni na utulivu “amesema Mgombea huyo urais.
Aidha, amesema kuwa katika siku 100 atakapoingia Ikulu uongozi atahakikisha anaunda tume ya mchakato wa mabadiliko ya katiba mpya ili kumaliza changamoto huyo ambayo ni kilio cha watanzania kwa muda mrefu.
“Ndani ya siku 100 za uongozi wangu nitahakikisha nasimamia elimu bure kuanzia ngazi ya awali hadi vyuo vikuu sambamba na kudhibiti mianya ya rushwa.
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→ http://Www.Cash43.Com