Puma Energy: Tunajifunza kupitia maoni ya wateja

DAR ES SALAAM: Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Fatma Abdallah, amesema kampuni hiyo itaendelea kuweka wateja kuwa kiini cha shughuli zake zote, ikiwa ni sehemu ya kujenga uhusiano imara na jamii inayohudumiwa.
Akizungumza wakati wa kuhitimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja 2025, yenye kauli mbiu “INAWEZEKANA,” Fatuma Abdallah alisema maadhimisho hayo yametoa nafasi kwa kampuni kutathmini huduma zake na kujifunza kupitia maoni ya wateja.

“Tunapohitimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja 2025 yenye kauli mbiu ‘INAWEZEKANA,’ nakumbushwa jambo moja muhimu katika kila tunalofanya wateja wetu,” alisema Fatuma Abdallah.
Ameongeza kuwa kampuni hiyo inaendelea kuhakikisha huduma zake zinazingatia ubora, uaminifu na ufanisi, huku lengo kuu likiwa ni kuimarisha maisha ya Watanzania kupitia bidhaa bora za nishati.

Katika wiki hiyo, timu ya Puma Energy ilifanya ziara katika vituo mbalimbali vya mafuta nchini, kukutana na wateja ana kwa ana, kusikiliza maoni yao, na kuwashukuru kwa kuendelea kuichagua kampuni hiyo kama mshirika wao wa kuaminika.

Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni, Puma Energy itaendelea kutoa bidhaa na huduma zenye viwango vya kimataifa, ili kusaidia maendeleo ya kiuchumi ya taifa kwa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi na uwajibikaji.



