MCC Asas: “Msiogope, tarehe 29 amani, kapigeni kura

IRINGA: MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri ‘Asas’, amewahakikishia Watanzania kuwa uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 utakuwa wa amani na utulivu, na kuwataka wananchi wajitokeze kwa wingi kupiga kura bila hofu.

Akizungumza katika mkutano wa kufunga kampeni za Ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, uliofanyika katika kata ya Isalavanu, tawi la Ugute, mbele ya maelfu ya wananchi, Asas alisema serikali imejipanga vyema kulinda amani ya nchi wakati wote wa uchaguzi.

“Ndugu zangu, msiwasikilize wanaotisha mitandaoni. Serikali imejipanga vyema kudumisha amani. Oktoba 29 nendeni kwa amani, mpige kura zenu bila woga huu ni uchaguzi wa amani na utulivu,” alisema Asas huku akishangiliwa na umati wa wananchi.

MCC Asas aliongeza kuwa, badala ya kuongozwa na hofu, wananchi wanapaswa kutumia siku hiyo kuchagua viongozi wanaoamini katika maendeleo, utulivu na umoja wa taifa, akiwataka wakipe kura Chama Cha Mapinduzi kuanzia ngazi ya urais, ubunge hadi udiwani.

“Rais wetu Dk Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa isiyopingika. Kazi zake zinajitosheleza kumpa kura za kishindo. Oktoba 29 tumpatie zawadi ya kura nyingi kama shukrani kwa uongozi wake wa hekima,” alisisitiza.

Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Mafinga Mjini kupitia CCM, Dickson Lutevele, alisema maendeleo yaliyotekelezwa chini ya uongozi wa Rais Dk Samia ni uthibitisho kuwa wananchi wanapaswa kuendelea kuiamini CCM.

“Tuna kiu ya maji, elimu bora, huduma bora za afya na uchumi unaokua. Nikipewa dhamana, nitapambana kuhakikisha haya yanatekelezwa kwa vitendo,” alisema Lutevele.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Tanzania limetoa taarifa rasmi likiwahakikishia wananchi kuwa hali ya usalama nchini ni shwari, na kwamba hakuna tishio lolote litakaloweza kuvuruga uchaguzi huo.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime leo, imeeleza kuwa jeshi limejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu katika maeneo yote nchini.

“Wananchi mnahakikishiwa usalama wa kutosha. Nendeni mkapige kura bila hofu yoyote. Tutadhibiti kwa mujibu wa sheria yeyote atakayejitokeza kuhatarisha amani ya nchi,” alisema Misime.

Taarifa hiyo imehitimisha kwa kusisitiza kuwa Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kwa yeyote atakayevunja sheria siku ya uchaguzi au baada yake.

Habari Zifananazo

5 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..

    .

    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. I’ve gained $17,240 only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, I was very troubled and thankfully I’ve located this project now in this way I’m in a position to receive thousand USD directly from home. Each individual certainly can do this easy work & make more greenbacks online by
    visiting following website….>>> https://www.Homeprofit1.site

  4. I’ve gained $17,240 only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, I was very troubled and thankfully I’ve located this project now in this way I’m in a position to receive thousand USD directly from home. Each individual certainly can do this easy work & make more greenbacks online by
    visiting following website….>>> https://www.Homeprofit1.site

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button