Amani yatawala Mtwara uchaguzi mkuu

MTWARA: MKUU wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala amewakikishia hali ya amani na usalama wananchi mkoani humo wakati wa Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.
Akizungumza leo Oktoba 27,2025 mkoani Mtwara, mkuu huyo wa mkoa amesema viongozi wao hao wamejipanga vema kuhakikisha hali ya amani na usalama inatawala kwenye mkoa huo.
“Ndugu wananchi sisi viongozi wenu wa mkoa tumejipanga vema kuhakikisha hali ya amani na usalama inatawala siku ya kupiga kura na niwahakikishie kuwa mkoa wetu hali ya usalama ni shwari,”amesisitiza Sawala.

Ameongeza kuwa: “Niwasihi nyote wenye sifa za kupiga kura mjitokeze kwenda kupiga kura kwa amani na utulivu kwani vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vipo kazini”.
Aidha, amewasihi wananchi hao baada ya kukamilisha zoezi hilo la kupiga kura wahakikishe wanaondoka eneo hilo la tukio ili wakaendelee na majukumu yao mengine ili kuepuka uvunjifu wa kisheria.
Ameendelea kuwasisitiza wananchi hao kuwa ushiriki wao katika kupiga kura utawapa fursa ya kikatiba ya kuchagua viongozi bora watakaoshirikiana nao kuleta maendeleo kwenye maeneo yao.




JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com