Ajira mpya 10, 919 Polisi, Magereza, Zimamoto, Uhamiaji zaja

DODOMA; WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imesema katika Mwaka wa Fedha 2026/27 inatarajia kuajiri watumishi wapya 10,919.
Kauli hiyo imetolewa bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Ncji, Patrobas Katambi akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya fedha ya wizara hiyo kwa mwaka 2026/27.
“Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2026/27, wizara inatarajia kuajiri watumishi 10,919.
“Kati ya hao, watumishi wa makao makuu ya wizara 249; Jeshi la Polisi 8,040; Jeshi la Magereza 1,046; Jeshi la Zimamoto na Uokoaji 500; Idara ya Uhamiaji 1,000 na NIDA 84,” amesema Waziri Katambi



