Daktari Rwamucyo kuhukumiwa leo

UFARANSA : MAHAKAMA mjini Paris imepanga kutangaza hukumu  dhidi ya daktari wa zamani wa Rwanda, Eugène Rwamucyo ambaye anatuhumiwa kushiriki katika mauaji ya kimbari ya Rwanda mwaka1994.

Waendesha mashtaka nchini humo wameiomba Mahakama kumfunga miaka 30 jela kwa Eugène Rwamucyo ambaye anatuhumiwa kwa mashtaka ya mauaji ya kiholela, kushiriki na kupanga kufanya uhalifu u dhidi ya binadamu.

Hatahivyo, upande wa utetezi umeendelea kukanusha tuhuma dhidi ya Eugène Rwamucyo,ambaye  hakuhusika na mashtaka yanayomkabili.

Advertisement

Mashahibi mbalimbali nchini Rwanda walisafirishwa  kwa ajili ya kutoa ushahidi kuhusu mauaji ya kutisha yaliyotokea katika eneo le Butare nchini Rwanda .

SOMAUfaransa yasafishwa tuhuma mauaji ya kimbari Rwanda

Hii itakuwa ni kesi ya saba tangu kusomwa na kusikilizwa  inayohusiana na mauaji ya halaiki ya Rwanda yaliyotokea mwaka 1994.