ZANZIBAR: RAIS wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi amevipongeza vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kwa kazi kubwa wanazozifanya kwa kuhakikisha amani na utulivu wa nchi, kushiriki kazi za uzalishaji mali , ujenzi wa miradi mbalimbali, kujenga uwezo na ujuzi kwa vijana , uanzishwaji wa viwanda, malezi kwa vijana na kuwafanya wawe wazalendo kwa mafunzo yanayotolewa, kutoa huduma kwa jamii ikiwemo elimu, tiba akitolea mfano wa hospitali ya KMKM.
Kamanda Mkuu huyo wa Idara Maalum ya Vikosi vya SMZ amesema hayo leo alipozungumza na Maafisa pamoja na Wapiganaji wa Idara Maalum za SMZ katika uwanja wa JKU-Kama Mkoa wa Mjini Magharibi.
Idara Maalum ya Vikosi vya SMZ inaundwa na JKU, KMKM, KVZ, Zimamoto na Uokozi pamoja na Chuo cha Mafunzo.