Dk.Talib ateuliwa Mwanasheria Mkuu Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amemteua tena Dk Mwinyi Talib Haji kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Zena Abdi imesema kuwa uteuzi huo umeanza leo 4 Novemba,2025.Dk. Mwinyi Talib Haji amepangwa kuapishwa alhamisi tarehe 6 Novemba, 2025 Ikulu Zanzibar. SOMA: Dk Mwinyi afanya uteuzi wa viongozi



