FDA yaidhinisha kidonge Wegovy kupunguza uzito

MAMLAKA ya Chakula na Dawa ya Marekani (FDA) imeidhinisha matumizi ya toleo la vidonge vya dawa ya kupunguza uzito ya Wegovy, hatua inayofungua ukurasa mpya katika matibabu ya unene kupita kiasi.
Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni ya dawa ya Novo Nordisk ya Denmark, idhini hiyo inaifanya Wegovy kuwa dawa ya kwanza ya kupunguza uzito katika mfumo wa kidonge kupata kibali cha FDA. Novo Nordisk imesema kidonge hicho kinachotumiwa mara moja kwa siku ni rahisi zaidi kwa wagonjwa ikilinganishwa na sindano, huku kikiwa na ufanisi unaolingana na toleo la sindano lililokuwapo awali.
Idhini hiyo inafuatia matumizi ya awali ya Wegovy kwa njia ya sindano baada ya FDA kuiruhusu kwa ajili ya kupunguza uzito. Katika majaribio ya kitabibu yaliyofanywa na kampuni hiyo, kidonge cha Wegovy kimeonyesha uwezo wa kupunguza uzito kwa wastani wa asilimia 16.6. SOMA: Mwenye kilo 145 afanyiwa upasuaji kupunguza uzito
Aidha, takribani theluthi moja ya washiriki wapatao 1,300 walioshiriki katika majaribio hayo walipunguza uzito kwa asilimia 20 au zaidi. Hadi sasa, Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) limesema limewasiliana na FDA kwa ajili ya kupata maelezo zaidi kuhusu idhini hiyo. Kidonge cha Wegovy kinatarajiwa kuanza kupatikana rasmi nchini Marekani mapema Januari 2026.



6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO
Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:
NO PROGRAMME
1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi
2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani
3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni
4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani
5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda
6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu
7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi
8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti
9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini
10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi
11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni
12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini
13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia
14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi
6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO
Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:
NO PROGRAMME
1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi
2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani
3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni
4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani
5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda
6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu
7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi
8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti
9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini
10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi
11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni
12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini
13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia
14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi