Fountain Gate yasaini dili nono na PigaBet

DAR ES SALAAM; TIMU ya Fountain Gate imeingia mkataba wa miaka minne na kampuni ya michezo ya kubashiri ya PigaBet kuwa mdhamini mkuu ili kuimarisha ushindani kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza Dar es Salaam jana wakati wa hafla hiyo Rais wa Fountain Gate, Japhet Makau alisema makubaliano hayo yana thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja na ya nalenga kuleta mapinduzi makubwa ndani ya timu hiyo inayokua kwa kasi.

“Nawashukuru PigaBet kwa uwekezaji huu mkubwa katika soka la Tanzania. Ushirikiano huu hau taisaidia tu Fountain Gate FC, bali pia utachangia ukuaji wa mpira wa miguu nchini kwa ujumla,” alisema Makau.

Aliongeza: “Ujio wao unaone sha wazi kuwa soka sasa ni chanzo muhimu cha ajira na fursa kwa vijana wetu”.

Makau alisema kuwa mkataba huo una kipengele maalumu cha motisha kitakachotolewa endapo timu itafanikiwa kumaliza katika nafasi tano za juu kwenye msimamo wa ligi.

Naye Meneja Masoko wa PigaBet, Arthur Kazora alisema kampuni hiyo imejizatiti kuunga mkono maendeleo ya michezo nchini na kushirikiana na Fountain Gate ni sehemu ya dhamira hiyo.

 

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. F8bet (hay F8 BET , F88BET) cổng game giải trí số 1 Việt Nam 2026 với nhiều khuyến mãi hấp dẫn. Trải nghiệm ngay để nhận lì xì vs code khủng

    1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
      .
      This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

    2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
      .
      This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button