Gaza yaongoza vifo vya wanahabari

BRUSSELS : WAANDISHI wa habari wapatao 104 wameuawa duniani mwaka 2024.

Taarifa hiyo imetolewa  mjini Brussels nchini Ubelgiji kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Wanahabari –IFJ, Anthony Bellanger amesema mwaka huu kumekuwa ongezeko kubwa la vifo vya wanahabari ukilinganisha na miaka iliyopita.

Bellanger amesema vifo vingi vya wanahabari  vimetokana kufuatia mizozo mbalimbali ya vita  inayoendelea kutokea katika mataifa  mbalimbali  kama huko Palestina ambapo waandishi wengi wameripotiwa kupoteza maisha..

Advertisement

Bellanger amesema  kuna wanahabari  wengine  ambao wamekamatwa  520 ambao mpaka leo wako gerezani bila sababu za msingi. SOMA: Watoto 260 wauawa vurugu Palestina

Maeneo yaliyotajwa kuongoza  kwa vifo vya wanahabari ni Mashariki ya Kati, Asia-Pasifiki na Ulaya hasa kutokana na vita vinavyoendelea nchini Ukraine.