Gonzalez aahidi mapambano

VENEZUELA : KIONGOZI wa upinzani nchini Venezuela Edmundo Gonzalez, ameahidi kuendeleza  mapambano  dhidi ya Rais wa Venezuela  Nicolas Maduro hata kama yuko nje ya nchi.

Gonzalez ambaye kwa sasa amekimbilia nchini  Hispania amesema ataendelea  kupigania demokrasia ili kuhakikisha Venezuela inaharakisha maendeleo yake.

Kiongozi huyu wa upinzani aliamua kukimbilia Hispania baada ya mahakama ya Venezuela kutoa waranti wa kumkamata.

Advertisement

Gonzalez aliwasili nchini Hispania hapo jana na serikali nchini humo imeshampatia hifadhi .

Marekani na nchi kadhaa za Amerika Kusini, zinaamini  Edmundo Gonzalez alishinda uchaguzi wa urais  uliofanyika Julai nchini  Venezuela .

SOMAPolisi wadhibiti maandamano Venezuela

Hatahivyo Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken, amesema hatua ya Gonzalez kuikimbia nchi yake ni kielelezo tosha cha sera zinazoenda kinyume na demokrasia nchini Venezuela.