Hali ni Shwari Ziwa Victoria

MWANZA: IMEELEZWA kuwa hali ya ulinzi na usalama ndani ya ziwa Victoria imeendelea kuimarika tofauti na miaka ya nyuma kutokana na  tathimini zilizofanyika kupitia vikao vitano vilivyohusisha Maofisa wa Jeshi la Polisi, maafisa uvuvi pamoja na taasisi nyingine zinazohusika na ulinzi wa rasilimali ndani ya ziwa hilo.

Taarifa hiyo imetolewa  Oktoba18,2023, na Mkuu wa Usimamizi wa Vikosi Maalum vya Polisi kutoka Kamisheni ya Opereseheni na Mafunzo, Makao Makuu ya Polisi Dodoma (DCP), Ferdinand Mtui katika kikao maalum kilichowakutanisha  Makamanda wa Jeshi la Polisi kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa na wadau wa uvuvi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Operesheni za Jeshi la Polisi Nchini, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Mihayo Msikhela amesema kuwa  katika kipindi cha mwaka 2019-2020 kuliibuka uhalifu ndani ya ziwa Victoria ikiwemo mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha, uporaji wa nyavu, samaki na boti za Injini.

SACP Mihayo aliongeza kuwa vitendo hivyo vilipelekea majeruhi na vifo kwa baadhi ya wavuvi na wafanyabiashara ziwani lakini kwa sasa matukio hayo yamedhibitiwa kwa kiasi kikubwa.

Aidha katika hatua nyingine SACP Mihayo aliongeza kuwa sheria za Nchi zimeweka bayana iwapo mtu akiingia Nchini kinyume cha utaratibu ikiwemo kukosa kibali cha kusafiria atakamatwa na kufikishwa mahakamani huku akiwasisitiza wavuvi wa Tanzania wasivuke mipaka ya ziwa Victoria  kwenda katika maeneo ya Nchi jirani za Kenya na Uganda.

Awali akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi ameeleza kuwa sekta ya uvuvi inachangia kwa asilimia saba ya pato la Mkoa.

Amesema kuwa Mkoa wa Mwanza umedhamiria kutekeleza mpango wa maendeleo wa miaka mitano katika sekta ya uvuvi ya kuifanya Mwanza kuwa na uchumi wa bluu kwa kuanzisha miradi mbalimbali kupitia ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba.

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
julia
julia
1 month ago

I’ve got my first check for a total of 13,000 dollars. I am so energized, this is whenever I first really acquired something. I will work much harder now and I can hardly hang tight for the following week installment.
.
.
Detail Here———————————————————->>>  http://Www.BizWork1.Com

Marry
Marry
1 month ago

We started Work with Google all the way from the beginning. Everybody can come in
together and work on these shared documents,(0) Join Work As Well Today And Take Income

Detail Here———————————————————->>> http://www.smartcash1.com

KellieEdwards
KellieEdwards
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by KellieEdwards
Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x