INEC yawafunda wasimamizi  86 Arusha, Manyara

ARUSHA; WASHIRIKI 86 kutoka Mikoa ya Arusha na Manyara, ambao ni waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi, maofisa uchaguzi na maofisa ununuzi  wanapatiwa mafunzo jijini Arusha.

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), inaratibu na kuendesha mafunzo hayo kwa watendaji hao maeneo mbalimbali nchini  ikiwa ni maandalizi kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.

Akifungua mafuzo hayo, Dk  Zakia Mohamed Abubakar, amabye ni Mjumbe wa INEC,  alisema watendaji hao wamepewa dhamana ya kusimamia na kuratibu uendeshaji  wa Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani  kwa Tanzania Bara,  ambapo ni jukumu kubwa na nyeti kwa mustakabali wa Taifa.

“Nawasisitiza kuwa mjitahidi na mjiepushe kuwa  vyanzo vya malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wa Uchaguzi, “amesema Dk Abubakari.

Amewataka watendaji hao  kufanya utambuzi wa vituo vya kupigia kura mapema, ili kubaini mahitaji maalumu ya vituo husika na kuhakikisha kunakuwa na mpangilio mzuri, ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani.

Amewasisitiza watendaji hao  kuwa wasome kwa umakini katiba, sheria,kanuni ,miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na tume

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button