Israel haijajibu kusudio la Hamas kusitisha mapigano

ISRAEL haijasema chochote kuhusiana na mpango wa kundi la wanajeshi wa Palestina Hamas juu ya kusitisha mapigano kwa siku nne kuanzia kesho Alhamisi.

Hamas wameeleza nia ya kusitisha mapigano hayo huku ikingoja kauli ya Israel kuhusu makubaliano.

Wakati Hamas wakiwa na kusudio hilo, Israel inataka kuachiwa kwa mateka wao wa kwanza na wanatarajia kuwapokea Alhamisi, Waziri ya Nje wa Israel, Eli Cohen ameeleza.

Chini ya makubaliano hayo, mateka 50 wa Israel waliotekwa na Hamas wataachiwa, wanawake na vijana 150 wa Kipalestina waliokuwa kwenye jela za Israel wataachiwa pia.

Familia za wale wanaoshikiliwa huko Gaza zimesema kila mateka “anahitaji kurudi nyumbani” na kwamba kila saa ni “muhimu”.

Israel imeendeleza operesheni yake ya ardhini na anga huko Gaza na msemaji wake mkuu wa jeshi amesisitiza kuwa vita vinaendelea.

Israel ilianza kushambulia Gaza baada ya wapiganaji wa Hamas kuvuka mpaka Oktoba 7 na kuua watu 1,200 na kuwachukua mateka wengine 240.

3 comments

Comments are closed.