Israel yaonywa mashambulizi Lebanon

WASHINGTON  DC : SERIKALI ya Marekani imeitaka Israeli kujiepusha na operesheni za kijeshi nchini Lebanon, baada ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kusema Lebanon inaweza kuwa kama  Gaza.

Huku Mkuu wa Jeshi la Israel, Herzi Halevi, akiahidi kuendelea kupiga ngome za Hezbollah ambapo mashambulizi hayo  yameua zaidi ya watu 1,200 tangu Septemba 23.

Netanyahu amewataka watu wa Lebanon kuiweka huru nchi yao kutoka kwa Hezbollah ili kuepuka vita vya muda mrefu.

Advertisement

SOMA : Jeshi la Israel laingia Lebanon

Rais wa Marekani, Joe Biden, alimshauri Netanyahu kuepuka kusababisha madhara kwa raia wa Lebanon, hasa katika maeneo yenye wakazi wengi kama Beirut.