Jeshi la Israel laua wapalestina 11

PALESTINA : JESHI la Israel limeshambulia eneo lenye uhitaji wa misaada ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza na kuwaua Wapalestina 11.

Shambulio hili limefanyika wakati jeshi hilo likipeleka magari ya kivita katika eneo la kaskazini la Jabalia wakati eneo hilo likiwa na hitaji kubwa la chakula.

Baadhi ya raia wa Jabalia wamesema jeshi la Israel limelipua nyumba kadhaa kwa mashambulizi ya angani, mizinga na kutega mabomu katika majengo.

Advertisement

Hatahivyo , vikosi vya uokoaji katika eneo hilo wamesema  watu kadhaa wamejeruhiwa ambao walijificha katika  shule moja iliyoshika moto baada ya kushambuliwa na kombora la Israel.

Kufuatia shambulio hilo, Jeshi la Israel limekubali kuruhusu  malori 50 ya msaada kuingia kaskazini mwa Gaza.

Wakati huo huo, jeshi la Syria limedai kuwa Israel imewajeruhi raia wawili na kuharibu kambi ya kijeshi mapema leo katika shambulizi lililofanywa kwenye mji wa pwani wa Latakia nchini humo.

SOMA: Mashambulizi ya Israel yanateketeza familia Gaza