Jokate – Nimejipanga kushirikiana na viongozi, wanachama

Ni baada ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu UWT

KOROGWE, Tanga: Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Jokate Mwegelo amesema ameupokea kwa unyenyekevu mkubwa na furaha kubwa uteuzi huo na kusisitiza kuwa amejipanga kushirikiana na viongozi na wananchama wote wa UWT.

Mwegelo ameandika mengi katika ukurasa wake saa chache baada ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kuteua kushika wadhifa huo baada ya kutumikia serikali kwa miaka kadhaa kama Mkuu wa Wilaya Kisarawe, Temeke na Korogwe.

“Nitumie nafasi hii kuishukuru Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake na Rais wetu Mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuniteua kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania ngazi ya Taifa.

“Ni heshima kubwa kuona Chama changu kikiendelea kutuamini Vijana na kutupa majukukumu makubwa ya kukitumikia Chama na Taifa. Naamini uteuzi huu utakuwa chachu kwa Mabinti wadogo Chipukizi wa Chama kupambania ndoto zao wakiamini wanacho Chama ambacho kinawajali na kuwaamini watu wote wenye uwezo na dhamira ya kweli ya kuleta mageuzi ya kweli na maendeleo ya Chama na Taifa letu,” ameandika Jokate. 

Jokate amemshukuru Mwenyezi Mungu, Familia yake, na Wananchi wa Korogwe kwa kumuombea na kumshika mkono. “Nimepokea meseji na simu nyingi za pongezi, nimezisoma pia comments zenu nzuri mitandaoni, nawashukuru sana.”

Amesema: “Nimejipanga kushirikiana na Viongozi na Wanachama wenzangu wote wa UWT kote nchini kwa uadilifu, ueledi, ubunifu, ustadi, uzalendo, umakini nikitanguliza mbele maslahi mapana ya Chama na Taifa ili kuendelea kuiimarisha Jumuiya yetu na kukijenga Chama chetu.”

Aidha, nipo tayari kushirikiana na Wadau wote wanaopigania Maendeleo na Ustawi Wanawake kote Duniani bila kujali tofauti zetu za Itikadi za Vyama, Dini, Utaifa, Kabila.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
MaryRobbins
MaryRobbins
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by MaryRobbins
MAPESA1234567
MAPESA1234567
1 month ago

HE/SHE DIED WITH CARDINAL RUGAMBWA HOSPITAL “CONFERENCE” DISEASE… THE HISTORY OF THIS DISEASE WAS KILLED MORE THAN 5 MILION PEOPLE AROUND THE WORLD MANY WAS CHINESE, EROPEAN, KOREAN AND INDIANS… ALL WHERE WHITE SKIN PEOPLE

MAPESA1234567
MAPESA1234567
1 month ago

HE/SHE DIED WITH CARDINAL RUGAMBWA HOSPITAL “CONFERENCE” DISEASE… THE HISTORY OF THIS DISEASE WAS KILLED MORE THAN 5 MILION PEOPLE AROUND THE WORLD MANY WAS CHINESE, EROPEAN, KOREAN AND INDIANS… ALL WHERE WHITE SKIN PEOPLE…. KILICHOBAKI BABA/BWANA YESU ASIFIWE DISEASE

money
money
1 month ago

ULIMWENGU WA NDOTO

One.  DEREVA BODABODA ANA NDOTO YA KUMILIKI KAMPUNI YA NDEGE

Two.    MUUZA MBOGAMBOGA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA MBOGA MBOGA

Three.             MUUZA VITUNGUU SUMU ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA VITUNGUU SUMU 

Four.  MUUZA NYANYA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NYANYA

Five.    MUUZA MAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NDEGE

Six.         MUUZA BAR ANA NDOTO YA KUMILIKI KUJENGA BAR

Seven.          MUUZA FREMU ANA NDOTO YA KUMILIKI SHOPPING MALLS

Eight. MGANGA WA KIENYEJI ANA NDOTO YA KUMILIKI HOSPITALI

Nine. MPIGA DEBE ANA NDOTO ZA KUMILIKI KAMPUNI YA MABASI

Ten.      MAMA NTILIE ANA NDOTO YA KUMILIKI HOTELS

Upo sahihi “tukasomeeeeeee tueleweeeeeee Saaaana

Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x