Kimbunga Milton chabisha hodi Florida

MAREKANI : KIMBUNGA Milton kimetuwa jimboni Florida na kusahabisha uharibifu mkubwa na kuacha takriban nyumba na maakazi milioni 3 bila ya huduma ya umeme .

Kampuni za nishati ya umeme zimeendelea kutoa huduma  kwa takriban watu milioni 11.5 huku idadi inayoongezeka ya watu wakiendelea kukosa umeme kutokana na kiwango cha juu cha upepo, dhoruba kali na mvua kubwa ikiendelea kunyesha kutokana na athari za kimbunga Milton.

Haya yanajiri huku Rais Joe Biden akimshambulia  Donald  Trump kwa madai ya kueneza taarifa za uongo  juu ya jinsi serikali yake ilivyolishughulikia suala la Kimbunga.

Advertisement

SOMA : Mamia ya watu hawajulikani walipo

Kimbunga Milton kimetuwa Florida na kinatajwa kuwa kikali na cha hatari zaidi, kikipiga kwa kiwango cha juu zaidi  ukilinganisha na Kimbunga Helene.