Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Tanzania Dk Samia Suluhu, pamoja na Katibu Mkuu wa chama hicho Daniel Chongolo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Christina Mndeme, leo Jumanne wamekagua maandalizi mbalimbali ya Mkutano Mkuu wa 10 wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Desemba 7-8, 2022 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.