Makamba awasili Uholanzi ziara ya siku tatu

fursa za biashara Tanzania na Uholanzi zatajwa

THE HAGUE: Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amewasili jijini The Hague, Uholanzi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Novemba 13-15, 2023.
Katika ziara hiyo Makamba ataongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi litakalofanyika Novemba 14 na 15 Jijini The Hague.
Aidha, pembezoni mwa kongamano hilo, Waziri Makamba atapata nafasi ya kukutana na Waziri mwenzake wa Mambo ya Nje wa Uholanzi, Kanke Bruins Slot. Kadhalika Makamba anatarajiwa pia kukutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Uholanzi (Tanzania Diaspora).
Waziri Makamba ameambatana na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dk. Tausi Kida na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Daniel Mushi.
Wengine wanaoshiriki kwenye ujumbe wa Waziri ni Mabalozi na Maafisa Waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Pamoja na Wakuu wa Mashirika mbalimbali Serikalini yanayotafuta ubia na mashirika ya Uholanzi.
Pia ujumbe wa Waziri Makamba umehusisha wafanyabiashara 16 kutoka sekta binafsi za Tanzania ambao watashiriki kwenye kongamano hilo.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
KareBacon
KareBacon
19 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 19 days ago by KareBacon
EmmaJames
EmmaJames
19 days ago

My last salary was $8,750 only worked 12 hours a week. My longtime neighbor estimated $15,000 and works about 20 hours for seven days. I can’t believe how blunt he was when I looked up his information.
.
.
Detail Here——————————————————>>>  http://Www.BizWork1.Com

Angila
Angila
19 days ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month i have earned and received $18539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money Online. Get this today by follow instructions……
.
.
.
On This Website……………..> > W­w­w.S­m­a­r­t­c­a­r­e­e­r­1.c­o­m

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x