Maonesho ujuzi, ajira yadhihirisha uwekezaji wa Uswis kwa vijana TZ

IRINGA: Naibu Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Nicole Providoli, ameshiriki uzinduzi wa maonyesho ya ujuzi, fani na ajira kwa vijana mjini Iringa, akiipongeza jamii ya Iringa kwa ukarimu na dhamira ya kweli katika kuliwezesha kundi hilo kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Taifa.

Amesema kati ya mwaka 2022 na 2025, serikali ya Uswisi imewekeza zaidi ya Sh Bilioni 23 kwa ajili ya kuwawezesha vijana wa Kitanzania kupitia mradi wa Skills for Employment Tanzania (SET) unaotekelezwa na taasisi ya Swisscontact, ikiwa ni sehemu ya kusaidia nguvu kazi ya taifa kwa kuwapatia maarifa, ujuzi na fursa za kazi.

“Tumefika Iringa tukiamini kuna fursa kubwa kwa vijana. Tunaona ni wakati sahihi kusaidia vijana waliomaliza shule na vyuo kutafsiri maisha kulingana na elimu waliyonayo na mahitaji ya ajira yaliyopo mtaani,” alisema Balozi Providoli.

Alisema wakiwa ni washirika wa maendeleo wa Tanzania wataendelea kufadhili mahitaji ya vijana ili kuwajengea uwezo wa kweli wa maisha na uchumi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Swisscontact nchini Tanzania, Rudolf Nuetzi, alisema maonyesho hayo ni jukwaa muhimu la kuwaleta pamoja waajiri, watoa mafunzo, taasisi za kifedha, serikali na vijana kwa ajili ya kujenga mfumo shirikishi wa maendeleo ya ajira na ujasiriamali.
Alieleza kuwa mradi wa SET umebadilisha maisha ya maelfu ya vijana nchini na kutoa mfano wa kijana kutoka Morogoro aliyekosa mwelekeo lakini kupitia programu hiyo sasa ameweza kuanzisha biashara na kuwaajiri vijana wengine wawili.

“Ni wakati wa vijana wa Iringa kuamsha fikra na kushinda changamoto zao kwa vitendo,” alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Astomini Kyando, alisema maonesho hayo si tu yanatoa elimu bali yanajenga fursa za maisha, ujasiriamali, mitandao ya kikazi na ushirikiano na taasisi mbalimbali.

“Maonesho haya ni mkombozi kwa vijana wetu. Yamewasaidia kuelewa ujuzi unaohitajika sokoni, kukutana na waajiri, wajasiriamali waliobobea, na taasisi za kifedha kwa ajili ya msaada wa mitaji. Tunawashukuru wadau wetu wa Uswisi kwa kuona thamani ya vijana wetu,” alisema DC Kyando.

“Niwashukuru Ubalozi wa Uswisi kwa kuendelea kuwa washirika wa kweli wa maendeleo. Mmechangia moja kwa moja utekelezaji wa sera zetu na maendeleo ya viwanda. Tunaikaribisha Swisscontact kuendelea kuwekeza katika sekta ya ujuzi hapa Iringa,” alisema.

Maonesho haya yaliyoandaliwa na Swisscontact kupitia mradi wa SET na kufadhiliwa na Ubalozi wa Uswisi, yamewakutanisha zaidi ya washirika 50 kutoka sekta ya umma, binafsi, NGOs, taasisi za mafunzo ya ujuzi na taasisi za kifedha.

Hadi sasa, zaidi ya vijana 3,000 wamehudhuria maonesho hayo ambayo yamebeba kauli mbiu isemayo:
“Kijana: Ujuzi Wako, Fani Yako, Chaguo Lako.”

Habari Zifananazo

6 Comments

  1. Wow that was unusual. I just wrote an extremely long comment but after I clicked
    submit my comment didn’t show up. Grrrr… well I’m not writing all that over
    again. Anyway,just wanted to say wonderful blog!

    Here is my website: Madeleine

  2. US Customs and Border Protection is paying General Dynamics to create prototype “quantum sensors,” to be used with an AI database to detect fentanyl and other narcotics. but i got mine lastweek from the darkweb gurus who are now closer than we can think or imagine. Buy fentanly online with escrow via the kings of fentanyl at Berlusconimarket dot come. or say berlusconimarket.com

  3. I honestly thought the days of reliable service were over when Berlusconi Market went dark. For years, I struggled to find a vendor that matched the quality and professionalism I grew accustomed to back in the day. When I heard Berlusconi Market (Berlusconimarket.com) was back in business, I was skeptical, but my recent order arrived on time and the quality is exactly as I remembered. so many people have missed the consistency that only Berlusconi Market could provide. They truly were the best back in the days of the darkweb, and it seems they haven’t lost their touch.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button