Marekani kusaidia tehama Tanzania

DAR-ES-SALAAM:  BALOZI wa Marekani nchini Tanzania, Dk. Michael Battle, amezipongeza juhudi za Tanzania katika matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano (Tehama) katika kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Akitangaza washindi watatu wa shindano la US-Tanzania Tech Challenge, Balozi Battle alisisitiza kuwa matumizi ya Tehama sasa ni muhimu, kwani kila kitu kiko mtandaoni.

Balozi Battle aliwataka washindi kutumia ujuzi wao wa Tehama kama fursa na kuwa jukwaa la kuhabarisha umma kuhusu rasilimali zilizopo mtandaoni kwa faida ya taifa.

Advertisement

“Hii ni fursa iliyo mbele yenu, ndoto ambayo nawashawishi muitafute na msikubali kukaribisha  ndoto ndogo, na kama una ndoto ndogo basi tafuta mwenye ndoto kubwa  ili akushawishi kubuni vitu vipya vya kuabdilisha  dunia “, alisema Dk. Battle

Aidha, Dk. Gerald Kafuku, Meneja wa Ubunifu na Teknolojia, aliongeza kuwa serikali inaendelea kuwekeza zaidi katika sekta ya habari na mawasiliano ili kuunga  mkono juhudi zinazofanywa na wabunifu chipukizi wa masuala ya Tehama na kufungua ya fursa za kiuchumi.

Alisisitiza kuwa COSTECH inashirikiana na wadau wa maendeleo kuwasaidia wabunifu wachanga katika kuleta mabadiliko chanya katika sekta mbalimbali nchini ili kuliwezesha taifa kusonga mbele.

“lengo la serikali kuibua  vipaji vya Tehama hasa ukizngatia ukuaji wa teknolojia ya habari na mawasiliano inakua kwa kasi sana  sasa imekuja akili mnemba  lazima  tukimbizane nah ii kitu”, Alimalizia  Dk. Kafuku

Washiriki zaidi ya 100 walionesha ubinfu wa miradi yao ya Tehama ambapo washindi nane waliingia  katika kinyang’anyiro cha kuchaguliwa  tatu bora.

SOMA : Samia aikaribisha Marekani uwekezaji maeneo matano

Jamii Forum aliibuka kidedea na kupatiwa $100,000 , mshindi wa pili Smart Foundry alipata  $80,000 na mshindi wa tatu  Launch Pad Tanzania alipata  $70,000.