Marekani Ufaransa kuijadili mashariki ya kati

 

UFARANSA: WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Marekani anayemaliza muda wake Antony Blinken ameanza ziara ya kikazi nchini  Ufaransa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka  Shirika la habari la AFP limesema kuwa lengo la ziara ni kutafuta ushirikiano kuhusu eneo lenye  misukosuko la Mashariki ya Kati.

Advertisement

Katika ziara hii,Blinken atakutana na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ambaye atamkabidhi nishani ya heshima ya juu zaidi ya Ufaransa.

Pia  atakutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot kwa mazungumzo yanayoangazia Mashariki ya Kati ikiwa ni pamoja na Syria.

SOMA: Blinken ataka amani Mashariki ya Kati