Matumizi mfumo NeST yaokoa bil 13.3/-

SERIKALI imeokoa zaidi ya sh bilioni 13.3, fedha ambazo zingetumika kwenye matumizi ya karatasi sambamba na kuondoa hewa ya ukaa takribani metariki tani 650 baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa Usimamizi wa Ununuzi wa Umma(NeST).

Pia tangu kaunzishwa kwa mfumo huo, makundi maalum wakiwamo vijana, wazee, wanawake na watu wenye ulemavu ambao hawana uwezo wa kufungua makampuni wamepatiwa zabuni zenye thamani ya sh bilioni 24.

SOMA: Wahamasishwa kuchangamkia fursa mfumo wa NeST

Amesema mfumo wa NeST,umekuwa na faida nyingi kwa taifa ikiwemo kupunguza muda na gharama za michakato ya zabuni za Umma, matumizi ya moduli ya usimamizi wa mikataba, kuweka uwazi na kutenda haki katika michakato ya ununuzi pamoja na kuongeza uwajibikaji kwa taasisi nunuzi na wazabuni.

“Pamoja na jitihada za serikali kuweka nyenzo za kidijitali,mafanikio ya upatikanaji wa thamani halisi ya fedha hayatapatikana kama wadau wote hatutazingatia uadilifu na uzalendo sote tunafahamu uadilifu ni kutenda kwa usahihi hata kama hakuna mtu yeyote anayekuangalia au kukufuatilia,” amesema.

Naye Meneja Ununuzi kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma(PSSSF), Gloria Nguge, amesema mafunzo hayo yatawajengea uwezo wa kujua moduli mbalimbali zinazofanyika kupitia kwenye Mfumo wa NeST.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button