Mchuano mkali ubunge ACT jimbo la Malindi

TAARIFA kutoka ndani ya Chama cha ACT Wazalendo zinaonesha jumla ya wanachama watatu wa chama hicho wamejitokeza kuchukua fomu za kuwania ubunge wa Jimbo la Malindi lililopo Unguja, Zanzibar.

Wanachama hao ni Katibu wa Chama hicho wa Mkoa wa Mjini, Maĥmoud Ali Mahinda, Waziri Kivuli wa Maendeleo ya Wanawake, Watoto na Makundi Maalum katika Baraza Kivuli la Mawaziri la ACT Wazalendo Zanzibar Halima Ibrahim na Mwanachama ŵa Çhama hicho Badru Adam Alì.




