Mikakati yawekwa kupaisha Soko la Kisutu

UONGOZI wa Soko la Kimataifa la Kisutu la mkoani Dar es Salaam unatarajia kuweka mabango makubwa kulitambulisha soko hilo kwa lengo la kuvutia zaidi wateja kwenda sokoni hapo.

Meneja wa soko hilo lililopo katika Kata ya Mchafukoge Wilaya ya Ilala, Happy Njovu alisema hayo alipozungumza na HabariLEO. “Tunategemea kuweka mabango makubwa ya kutambulisha soko letu,” alisema.

Njovu alisema pamoja na jitihada hizo, pia wanawarudisha sokoni wafanyabiashara wanaokwenda mtaani kufanya biashara zao.

Alisema Kisutu ni soko la kimataifa kwa sababu limekuwa likihudumia watu tofauti kutoka kwenye balozi na lipo mjini.

“Bidhaa zinazovutia kwenye soko letu ni mbogamboga na matunda kwa sababu ukija kwenye soko la Kisutu utakutana na mboga ambazo inawezekana huzifahamu na matunda adimu ambayo si rahisi kuyapata katika masoko mengine ya Dar es Salaam,” alisema.

Alisema kwa sasa soko hilo lina wafanyabiashara 1,060 na uwezo wake ni kuchukua wafanyabiashara zaidi ya 1,500.

Katibu wa bidhaa ya matunda sokoni hapo, Mustapha Nyinga alisema soko hilo linauza matunda tofauti ambayo hayapatikani kwenye masoko mengine ya kawaida.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
jedites
1 month ago

My last month paycheck was for 11000 dollars… All i did was simple online work from comfort at home for 3-4 hours/day that I got from this agency I discovered over the internet and they paid me for it 95 bucks every hour…..>
 https://www.pay.salary49.com

Money
Money
1 month ago

Taulo za kike na VITU VYA KWETU

Tangazo.PNG
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x