Msumbiji wapanga maandamano

MSUMBIJI : TUME ya uchaguzi nchini Msumbiji inatarajiwa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa rais na bunge uliofanyika 9 Oktoba mwaka huu.

Kwa sasa hali ya wasiwasi imeongezeka nchini humo kabla ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa ambayo yanatarajiwa kutangaza ushindi wa  chama tawala cha Frelimo.

Hatahivyo, Rais Filipe Nyusi  amewaambia waandishi wa habari kuwa hatua ya kuchochea umma kufanya maandamano  kutatengeneza  mazingira ya vurugu  na  ni suala ambalo litaangaliwa kama uhalifu.

Advertisement

Naye Mgombea wa upinzani, Venancioa Mondlane, ameamua kuitisha maandamano ya  siku 25 kupinga  mauaji ya wakili wake  Elvino Dias aliyepigwa risasi mara 25 na vikosi vya usalama nchini humo.

SOMA : Picha: Rais Nyusi ahitimisha ziara nchini