Mwigulu: Dira 2050 Ni Ajenda ya Taifa

WAZIRI Mkuu Dk.Mwigulu Nchemba ameagiza kuanza mara moja utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050 kupitia Mpango na Bajeti ya Serikali, akisisitiza ushirikishwaji wa sekta binafsi na wadau wa maendeleo ili kuharakisha ukuaji wa uchumi jumuishi na shindani.
Dk. Mwigulu ametoa maagizo hayo Aprili 1, 2026, Bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha hotuba ya mapitio na mwelekeo wa kazi za Serikali pamoja na makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2026/2027.
Ameitaka Tume ya Mipango kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu Dira 2050 ili kuongeza uelewa na ushiriki wa wadau katika utekelezaji wake.Amesema Dira hiyo iliyozinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan Julai 17, 2025, inalenga kujenga Taifa jumuishi, lenye ustawi kwa wote, haki na linalojitegemea ndani ya kipindi cha miaka 25 ijayo. “Nitoe rai kwa viongozi wa Serikali, dini, sekta binafsi na asasi za kiraia kuhakikisha mipango yao inawiana na vipaumbele vya Dira 2050,” amesema.

Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, utekelezaji wa Dira hiyo unalenga kufikisha uchumi wa Taifa kufikia dola trilioni moja na pato la mtu mmoja mmoja kufikia dola 7,000 kwa mwaka ifikapo 2050. Ametaja nguzo muhimu za kufanikisha malengo hayo kuwa ni utawala bora, amani, usalama na matumizi bora ya rasilimali za Taifa ili kupunguza utegemezi wa nje.
Aidha, amesema Dira 2050 imejengwa katika nguzo tatu kuu ambazo ni uchumi imara, jumuishi na shindani; maendeleo ya watu na jamii pamoja na uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi. Katika utekelezaji wake, Serikali imeweka mikakati mbalimbali ikiwemo kuimarisha ubia kati ya sekta ya umma na binafsi, matumizi yenye tija ya rasilimali pamoja na kukuza utamaduni wa kuweka akiba kwa ajili ya uwekezaji.
Amesema Mpango na Bajeti ya mwaka 2026/2027 ni hatua ya kwanza ya utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/2027–2030/2031) wenye dhima ya “Mageuzi katika Kukuza Uchumi na Kuzalisha Ajira.”Pia, Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na tathmini ili kuhakikisha uwajibikaji na utekelezaji wenye tija wa Dira hiyo.SOMA: Wabunge BLW waapishwa, wabainisha vipaumbele
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameliomba Bunge kuidhinisha shilingi trilioni 12.50 kwa ajili ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake, ambapo trilioni 8.73 ni matumizi ya kawaida na trilioni 3.76 ni ya maendeleo. Aidha, ameomba kuidhinishwa kwa shilingi bilioni 225.02 kwa Mfuko wa Bunge, zikiwemo bilioni 207.99 kwa matumizi ya kawaida na bilioni 17.03 kwa ajili ya maendeleo.




Makes $200 to $240 reliably online work and I got $16894 in One Month electronic acting from home. I am a modest piece at a time understudy and work in a general sense one to a few hours in my extra time. Everybody will finish that obligation and makes online additional money by basically open this link
HERE ➤➤ www.work27.online
JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com
I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
.
This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com