Namungo kuijaribu KMC Ligi Kuu leo

KLABU ya Namungo ya mkoani Lindi leo inashuka dimba la KMC Complex, Dar es Salaam ikiwa mgeni wa KMC katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

KMC ipo nafasi ya 9 katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 11 baada ya michezo 9 wakati Namungo ni ya 12 ikiwa na pointi 9 baada ya michezo 9 pia.

SOMA; KMC msimu ujao ligi kuu kama kawa

Advertisement

Katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu uliopigwa Oktoba 30, bingwa mtetezi Yanga imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kushinda mchezo wa 8 mfululizo ikiifunga Singida Black Stars kwa bao 1-0 lililofungwa na Pacome Zouzoua dakika ya 67 katika uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Kwa matokeo hayo Yanga inaongoza ligi ikiwa na pointi 24, haijapoteza wala kutoka sare mchezo wowote.