Rais Mwinyi azindua Mji wa Dk. Hussein Mwinyi

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameuzindua rasmi Mji wa Dk. Hussein Mwinyi uliopo Mombasa, Mkoa wa Mjini Magharibi, na kuutaka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) kuendelea kujikita katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo yenye tija kwa Taifa.

Rais Dk. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo, Desemba 23, 2025, wakati wa uzinduzi wa mji huo wa kisasa uliofanyika katika kuadhimisha Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Amesema mifuko ya hifadhi ya jamii imekuwa nguzo muhimu ya maendeleo katika nchi nyingi duniani, huku akiipongeza ZSSF kwa kuanza vyema utekelezaji wa mradi huo mkubwa, hususan katika ujenzi wa makazi ya kisasa na ya gharama nafuu kwa wananchi.

Aidha, ameitaka ZSSF kuongeza wigo wa uwekezaji kwa kujikita zaidi katika miradi mikubwa ikiwemo miradi ya uzalishaji na usambazaji wa nishati ya umeme, baada ya mafanikio iliyoyapata katika ujenzi wa masoko, vituo vya mabasi na nyumba za makazi.

Rais Dk. Mwinyi amesema Zanzibar inahitaji kuwa na miji mipya ya kisasa yenye hadhi na ubora ili kuwawezesha wananchi kuishi katika mazingira bora na salama. Ameeleza kuwa bado wapo wananchi wengi wanaoishi katika makazi duni na maeneo yasiyopimwa, hali inayosababisha changamoto za kimazingira na upangaji wa miji. SOMA: Mwinyi Azindua Miradi ya Maendeleo Zanzibar

Kutokana na hali hiyo, amewataka wananchi kuunga mkono juhudi za Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kuboresha maisha yao. Sambamba na uzinduzi wa mji huo, Rais Dk. Mwinyi pia amezindua nyumba za gharama nafuu pamoja na msikiti mpya uliojengwa katika eneo hilo ujulikanao kama Masjid Balad Salaam.

Ameitaka ZSSF kwa kushirikiana na wakaazi wa Mji wa Dk. Hussein Mwinyi kuhakikisha wanazitunza nyumba hizo ili ziendelee kuwa na haiba na ubora kwa muda mrefu. Vilevile, Rais Dk. Mwinyi ameridhia ombi la ZSSF la kupatiwa eneo kwa ajili ya ujenzi wa ofisi katika Mji wa Serikali Kisakasaka, na kuiagiza Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi kuipatia taasisi hiyo eneo la ardhi kwa ajili ya ujenzi huo, huku akisisitiza ofisi zitakazojengwa ziwe bora na za mfano.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. 6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO

    Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:

    NO PROGRAMME

    1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi

    2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani

    3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni

    4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani

    5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda

    6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu

    7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi

    8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti

    9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini

    10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi

    11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni

    12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini

    13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia

    14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi

  2. 6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO

    Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:

    NO PROGRAMME

    1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi

    2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani

    3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni

    4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani

    5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda

    6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu

    7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi

    8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti

    9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini

    10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi

    11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni

    12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini

    13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia

    14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button